Tuesday, August 2, 2016

JE NIFUNGUE KESI MAHAKAMA GANI KWA HAWA WANAONICHOCHEA KUA MUHALIFU?

JE NIFUNGUE KESI MAHAKAMA GANI KWA HAWA WANAONICHOCHEA KUA MUHALIFU?

Na C.P Lekule
Huyu mtu hanikwazi peke yangu kwa kauli zake,je ule mfano wa msichana akibakwa kama mavazi yalikua yanachochea yeye kubakwa naye anapewa adhabu hapa je haiwezi kutumika hiyo sheria,mimi kiukweli kuna baadhi ya viongozi wa nchi wananishawishi kuwa gaidi,yaani nakua na msukumo hadi wa kujiunga na vikundi viovu, je nikawashtaki wapi hawa wanaopekekea mimi kuwaza maovu? Je hakuna wakunishauri kesi yangu niipeleke wapi,na kuna mmoja wao nasikia hatakiwi kushtakiwa basi bashauri ambaye hashtakiwi na akifanya jambo yeye ni sahihi,basi hata yeye asiwe na haki ya kushtaki;_ naomba nizungumze ninachokijua mpaka sasa viongozi baadhi wa ngazi za juu ccm, wanajifunza namna ya kuijua hasira yangu,mimi ni mtanzania nina sumu ya amani mda mrefu,mkiigeuza kua vita ni kali zaidi ya sumu ya nyoka, namkumbuka wajina langu kabla hajafariki aliniambia,kuvunjika kwa mlango viti na meza uhofia,pia pia akaniambia paka halii nyau mpaka asikie harufu ya samaki au amuone samaki,bado naelezea ukurasa huu una maana kwa wenye akili ya grade A
Leo katika kurasa yangu ninaongezea kufafanua maana ya neno siasa,hapo zamani tulifunzwa na tukaelezwa pamoja na vitabu vingi kua maana ya neno siasa ni.
"... mawazo, mipango na busara za kuendesha nchi au jambo lolote". Kutokana na tafsiri hiyo basi ni dhahiri kua kila sekta tanzania inahitaji siasa ,kilichonifanya niandike hii nimeona watu wengi,wakifata mkumbo na kulitafsiri neno siasa vibaya,kuna madokta,walimu,maaskari,watu wenye elimu ya juu wamekua wakikosa adabu ya kutafsiri neno hili na kuliharibu siku hadi siku, ukizungumza jambo kwa maelezo mazuri sana utaambiwa unafaa kua mwanasiasa hiyo ni kweli,na pia ukiwa mpigania ukweli utasikia watu wanasema yule mwanasiasa ni kweli,ila sasa unapomkosoa mtu kwa kutumia haki utaambiwa usinichanganye na siasa zako,utasikia watu wanasema taaluma sio siasa tena watu wenye akili,huwa nasikitishwa sana watu wameshindwa kujua taaluma yoyote ni siasa,siasa iko kila mahali,siasa ndio maisha ya kila siku.Ndio maana mwalimu Nyerere akasema "siasa ni kilimo" sasa nashangazwa na raisi wa awamu hii kua dikteta hadi kwenye kiswahili,eti anasema siasa zinakwamisha maendeleo,bila kujua hata yeye yuko kwa ajili ya siasa,nimelazimishwa na watu kurudia kurasa hii,kwani tanzania inapoteza dira kwa kila jambo,raisi amekua msemaji wa kila wizara,na kutumia polisi kuwahujumu na kuwatisha wapinzani,wasiikosoe nchi hatutoacha kusema,kwani raisi alitakiwa kuiongoza nchi,na sio kuitawala kama anavyofanya sasa, mimi napenda kumuheshimu kiongozi yoyote anaeongoza kwa haki sio kidikteta, demokrasia ipo ila haitumiki vizuri,mimi ni kati ya watu wanaochukia kauli ya wengi wape,kwani tanzania tumekua tukiwapa wapumbavu wengi mamlaka ya kutuendesha kijinga na bado tunatulia tu.
Na kusema chaguo la Mungu tunamdhihaki Mungu kila kukicha,sio Tanzania tu afrika imekua ya ajabu sana, kwa sababu kila mtu amekua akimtegemea mwenzie aseme jambo,hata kama jambo linamuumiza atashukuru tu,ila mimi sikulelewa kusema nyeupe ni nyeusi,napenda kusema nyeupe ni nyeupe na nyeusi inabaki kua nyeusi tu, polisi wa Tanzania fanyeni kilicho haki sio kupelekeshwa na mtu fulani,itafika mahali tutaheshimiana tu, nitasimamia ukweli tu mara zote,na sitaacha mpaka nchi iwe kwenye mwelekeo wa haki,

Wananchi Hawajaribiwi

Naomba Mh.Raisi Maghufuli kama haupendi kujaribiwa na Wananchi pia hawapendi kujaribiwa,tena ukiendelea kuwajaribu hawa wananchi wakibadilika utajutia kua Raisi wa Tanzania,na wala hufuati nyayo za mwalimu Nyerere na wala huwezi,mambo mengi unakurupuka,nchi haiendeshwi kwa matamko hata siku moja,acha kuajiri watu kwa kukurupuka,nasema hivyo kwa sababu umekua ukiajiri watu masaa machache umewatengua,maana yake umekurupuka,unawanyima haki wapinzani,kwa sababu unawaogopa kiutawala,yaani unatakiwa uelewe kua raisi sio kwamba una akili zaidi ya wananchi wote,elewa kuna wenye akili zaidi yako, hivyo usituongoze kama umetawala Matahira tafadhali,siku machafuko yakitokea kwa kusababishwa na utawala hohehahe utawajibishwa kimataifa kinga haitasaidia,unaemkandamiza,unayemnyanyasa,unayemnyima haki siku akijua hakutakalika nchi itakua ndogo sana hii japo ni kubwa,mtu asiependa kukosolewa ana udhaifu wake mkubwa,hajui kuongoza anakua anahofia ubaya kuzidi wema wake,hakuna mwenye haki miliki ya nchi hii,tunakuomba kama ulichaguliwa halali, ongoza si utawale enzi za ufalme zilishaisha,acha kuweka historia mbovu katika nchi yetu,tunaumia kwa sababu nchi hii sio yetu peke yetu kuna vizazi na vizazi vijavyo, sio kila anaekosoa serekali apewe kesi ya uchochezi, Mwalimu Nyerere na wenzake wawili enzi za chama kimoja waliwahi kushtakiwa kwa kosa la uchochezi baadae kukaja vyama vingi sheria ilitakiwa kurekebishwa ila bado,HATARI YAJA TUSIPOKUA VIONGOZI MAKINI.

Monday, July 4, 2016

Saturday, July 2, 2016

KILIMANJARO by CV


KUTOKA KWA CP Lekule
KWENDA KWA ;_Waziri wa utalii
               Mh.Jumanne Magembe

YAH;KAZI ZA MSIMU HASA GUIDE NA POTER MLIMA KILIMANJARO.
Barua kwako waziri wa utalii JUMANNE MAGEMBE
Uandishi wa bazua za wazi untumika sana zama hizi Mh.enzi zile ilikua ngumu kwa sababu ya utandawazi kutokuwepo,tulikua tunatumia majani,karatasi,mawe na hata magome ya miti kufikisha ujumbe fulani mahali,ila siku hizi mambo mepesi kabisa,ni jambo la heri sana pia kwetu kufikisha mambo kadha wa kadha,kwa viongozi mbali mbali,natumaini yoyote atafikisha ujumbe huu kama hautakua online leo au kesho,kichwa cha habari hapo juu chahusika,
UTANGULIZI;_kama unavyoelewa kazi hizi zilivyo ngumu,muheshimiwa,ila kwa ufafanuzi mdogo tu,utafahamu
Nilianza utalii 2003 nikiwa kama mpagazi nilikua nikienda shule na baadae natoroka kuelekea kwenye kazi hiyo kupata matumizi madogo madogo na ada

Tulipambana kiukweli ila kila penye mkusanyiko walaji hawakosekani kazi hii ya kubeba mizigo ya watalii kwenda mlima kilimanjaro ni ngumu sana kiasi kwamba heri hata jeshini yaani namaanisha ukiwakusanya waliozoea ile kazi ukawapeleka jeshini wataona wako mapumzikoni, kipindi hicho kila kampuni zilikua na malipo tofauti ila mimi nilikua napanda na kampuni iliyokua inalipa elfu kumi na tano 15000 kiukweli ilikua hela kubwa sana na nilikua nina uwezo wa kufanya
kazi chache tu nikalipa ada na kumaliza matumizi mengine,ila baada ya mda lilianzishwa shirika lililodai ni la kutetea wapagazi na kua linachukua au linamega kiasi cha mshahara wa wapagazi eti kwamba ukifa watakusaidia au ukiugua,tulipambana na waanzilishi wa lile shirika kwani ulikua ni utapeli
Kwani sikuona kua linamsaada wowote lilikua ni kupe kwa wapagazi.

Kwa sababu kazi ile ni ya msimu na ndio maana kuna low season na high season,hivyo fedha zetu walizokua wanachukua hazikua na faida kwetu wakanitishia watanifunga,sikuchoka kuhoji naviongozi ambao pia nawafahamu kwa majina wa Kilimanjaro Nation Park walikua ndio wanawapa nguvu hawa matapeli kwa kujua au kutokujua mara ghafla baada ya shirika hilo kujikusanyia fedha za kutosha likapotea ghafla minongono mingi sana ilibaki japo wapagazi walisahau kutapeliwa kule na kuendelea na  kazi zao za msimu mara baada ya mda liliibuka tena likijiita Kilimanjaro Poter Asociation bado wakapewa nguvu kubwa zaidi na viongozi baadhi wa Kilimanjaro Nation Park pamoja na baadhi ya matour operators baadhi kwa maslai yao binafsi,na wengine mkumbo ili waitwe viongozi,kwa hili lazima kuna faida waliyokua wanaipata kwenye hilo shirika ninaloliita halikua likitenda haki lakini bado sikukaa kimya nilihoji na nikaonekana mkorofi, kama ilivyo tanzania ukiongea ukweli unachukiwa mkorofi.Sasa kwa mpagazi kukipata kitambulisho yaani kukipata kitambulisho ilikua 15000 bila kitambulisho huingii msituni,hubebi mzigo(chamanda,gas,mburuta na nk) ndio kauli ya yaani kitambulisho kinachoitwa cha  KPA ndio kinachohitajika sio cha kura wala mkazi, badala wapambane namna ya hawa wapagazi kupata stahiki zao wanahangaika kupunguza stahiki za wapagazi kwa kushirikiana na viongozi baadhi wa KINAPA,

Mashirika yako zaidi ya moja ada yao ni zaidi ya elfu 40 kwa miezi sita bado wanahitaji ujiunge na bima na uikorokoro kibao, hapa najiuliza kujiunga na shirika lolote duniani kikatiba ni hiyari je mbona huku ni lazima na kwanini KINAPA CHINI YA TANAPA MNAHALALISHA HUU UNYONYAJI KWA KAZI ZA MSIMU? kwa nini nasema kinapa chini tanapa wanashiriki hawa ndio sapoti ya hawa wanaotengeneza mashirika ya kinyonyaji, mimi najiuliza kuna maana gani ya kuweka mafunzo ya  uongozaji wageni na kutoa leseni ilihali ukija na mgeni leseni haina maana tena unaulizwa kitambulisho cha shirika lingine,kwanini kila tour operator au kampuni yenye tin number zisifanye haya mambo peke yao kwa sababu kila kampuni ina usajili wa wao.goza wageni na wapagazi wake na hata waongoza wageni kipindi cha mafunzo ya kitalii matour operator au kampuni ndio hutoa majina na yakapitishwa na KINAPA na sio shirika KGA au hayo mengine, kiukweli mimi mnanichanganya bado pamoja na barua hii nitakuja kwenye ofisi zenu tuzungumze tena ili nifahau nisichokijua na nyinyi pia mfahamu msichokijua

Funzo Kwa kizazi cha Utawala

Na CP Lekule
Tatizo kubwa nimeliona,wenye macho ambao kwa bahati nzuri ni wengi zaidi ya vipofu, nao nadhani wameliona,wapo walioliona wakashindwa kulisema japo wanatamani kusema,wengine wanakuja chinichini nakutuombia tuseme sisi tuliojaliwa kutokua na dhambi ya woga kwa mtu bali kwa Mungu tu,mtu unaposhindwa kua na watendaji wazuri,huenda hata sehemu uliyopo  ni bonge la suprise kwako so unashangaa kuapale ulipo kwani hukupatarajia hivyo unashangaa shangaa huku siku za utendaji zikiyoyoma,kwani ni sawa na mtu ambaye alikua hawazi kabisa kua hata boyfriend wa mtu leo hii anashangaa yuko kanisani au msikitini anafungishwa ndoa,pia kuna kiongozi hajawahi kuota hata siku moja kua mwenyekiti wa kitongoji, leo hii anashangaa kutajwa kiongozi wa ngazi ya juu, mfano mkuu wa wilaya,mkuu wa mkoa,mbunge,waziri,spika,naibu spika, na nk. Sasa ubaya wa uongozi unaoupata kua surprise ni kujikuta unapoteza weledi wa uongozi,na ndipo unapotofautiana na wenzako kwa kujiona wewe ndio wewe,wewe ndio final say wa kila kitu,kila jambo linahitaji maandalizi,viongozi wengi wazuri waliandaliwa,sasa mfano viongozi wa kwenye madhehebu mbalimbali na nk, Mwalimu nyerere hakukurupuka tu na kujikuta baba wa taifa,Amani Karume pia vivyo hivyo, achana na hao wa hapa wakina Kwame Nkuruma,Adolf Hitler,Saadam Husen,Gadafi na wengine kibao waliandaliwa hawakufanyiwa surprise kama viongozi wengi wa ccm walivyofanyiwa surprise,tuje kwenye maandalizi ya uongozi,kiongozi unaweza andaliwa na matatizo yanayoibuliwa ndani ya nchi,na viongozi wa namna hii huwa na vision kubwa ya kumlinda kila mtu,kiukweli kiongozi wa maandalizi ya namna hii huwa mzuri zaidi ya maandalizi yote,viongozi wa namna hii mara nyingi hupenda haki na mara nyingi nchi nyingi hushindwa kuhujumu nchi iliyotawaliwa na viongozi wa namna hii,hatimaye yanapotokea machafuko yoyote viongozi wa namna hii huweza kushinda kwa maana ya kwamba uzuri wao ndio huanza kujulikana zaidi na hata wapotezapo maisha hawafutiki katika historia.

Kuna viongozi ambao huandaliwa kindugu au kichama kwa kuandaliwa kwa namna hii,hakudumu sana katika uongozi,kiongozi wa namna hii mara nyingi hujikuta wanatawala kifalme badala ya kuongoza na nchi nyingi huingia kwenye machafuko au vita na mara nyingi hawaishindi vita,viongozi wa namna hii wengi hupinduliwa kijeshi,huwa hawakubali kung'ooka,viongozi wa namna hii huwa na vision ndogo tu hasa huwa na malengo na ndugu au chama na huwa na dharau mara nyingi,pia hua wanajitoa sana kuwalinda waliowaweka kwenye huo uongozi,hujaribu kulazimisha kua wao ndio wanaweza zaidi,kuliko wengine,huwafanya matajiri wakubwa wanaoshika uchumi kua upande wao,na wakionekana wako kinyume,huuwawa au kufungwa gerezani kwa mda mrefu sana,ili kuwapotezea vision,hutaka kuabudiwa japo maranyingi hufanya kinyume cha sheria, je tunaona nini tukiangalia kesho bila haraka,na tukiangalia kesho kwa haraka haraka,machozi tumeshayaona,jasho pia damu,je tunayoyafanya ni kwa ajili yetu peke yetu? Mzalendo hupigana kwa ajili ya kizazi kijacho,yu heri ateseke ila mwanae au mjukuu wake aishi kwenye amani,je kuna mtu anapigana kwa ajili ya watoto wake au ndugu waje kuishi vitani? Mzalendo hukubali kuishi vitani ila baadae wanaofuatia waishi kwa amani, mimi nitasimamia ukweli japo ukweli unawaumiza wanafiki wengi,viongozi wanaowajengea wananchi nidhamu ya woga,sio viongozi,pia kiongozi anayependa kukosolewa ndie kiongozi mzuri,ila anayeogopa kukosolewa huyo kashapima kua hana uwezo wa kukaa alipo,MUNGU ibariki Tanzania.

Saturday, May 21, 2016